skip to Main Content

16 June 2024, 9:20 am

viti mwendo vilivyotolewa na injinia Ismaili kwa wanafunzi wa shule za msingi wenye ulemavu manispaa ya Mpanda.picha na Ben Gadau

Na Ben Gadau -Katavi

Mdau wa maendeleo injinia Ismaili ametoa msaada wa viti mwendo 13 kwa watoto wenye ulemavu kwa shule za msingi manispaa ya mpanda mkoani Katavi

Akizungumza wakati wa kukabidhi viti hivyo Eng Ismaili amesema kuwa ameguswa na changamoto ambayo watoto hao wamekuwa wakiupata wakati wanaenda shule kupata elimu.

Kwa upande wake mwenyekiti wa shirikisho la watu wenye ulemavu Prasido Kameme ameshukuru baada ya kupokea viti hivyo huku akiendelea kuwaasa watu wengine kuiga mfano huo.

Wazazi na walezi wa watoto hao wameshukuru huku wakisema viti hivyo vitawarahisishia watoto hao kufika shuleni kwa urahisi kupata elimu.

Viti hivyo vyenye thamani ya shilingi milioni 6 na laki 7 vimetolewa kwa watoto wa shule za msingi Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi ambapo vitawasaidia katika kupata elimu.

Back To Top