Waombolezaji wakiaga mwili wa binti aliyeuawa. Na Anna Milanzi -Katavi Kufuatia mauaji ya Irene Yosia…

Na Samwel Mbugi
Mwanaume mmoja mwenye umri kati 60 – 65 ambaye jina lake limehifadhiwa amepigwa na kuvunjwa mguu na mke wake baada ya kutokea ugomvi baina yao.
Akizungumza na Mpanda Redio FM dada wa majeruhi amesema kuwa alifuatwa na mtoto kwa ajili ya kwenda kumsaidia baba yake ambaye alikuwa anavuja damu na baada ya kufika alikuta kaka yake amevunjwa Mguu.Sauti ya Dada wa majeruhi
Hata hivyo Mpanda Redio FM haikuishia hapo imefanya jitihada za kumtafuta mwenyekiti wa mtaa wa Kivukoni Jastine Michael ambaye nae amesema alipigiwa simu na dada wa mgonjwa akihitaji afike eneo la tukio na baada ya kufika alikuta damu zikivuja na kuamua kuchukua hatua ya kumpeleka hospital kwa ajili ya matibabu.Sauti ya mwenyekiti wa mtaa wa Kivukoni Jastine Michael
Hata hivyo Majeruhi ambaye alipigwa na mke wake hakuwa tayari kuzunguzia tukio hilo ambapo amesema atalizungumzia baada ya wiki mbili kupita.
