skip to Main Content
This image has an empty alt attribute; its file name is dsc-0346-1024x683.jpg

Mrindiko ameagiza kuhakikisha malengo ambayo yanapangwa yanafikiwa Kwa wakulima kufuata mbinu za kilimo, na wataalamu kuhakikisha tathimini inafanyika ili kulinganisha na misimu mingine na kwanini imekuwa vigumu kufikia lengo la kuzaliza Tani milioni 50″ Picha na Festo Kinyogoto

Na Festo kinyogoto-katavi

Wakulima wa zao la Pamba tumbaku na mazao mchanganyiko Mkoani katavi wamehakikishiwa soko la Uhakika la mazao hayo pamoja na malipo Kwa wakati Ili kujikimu na kukuza uchumi.

Hayo yamesemwa na mkuu wa mkoa wa katavi Mhe. Mwanamvua Hoza Mrindiko Katika hafla ya uzinduzi wa msimu wa masoko ya Pamba, tumbaku na mazao mchanganyiko  iliyofanyika Katika kijiji Cha Makongoro kata ya Magamba halmashari ya Manisapaa ya Mpanda Mkoani katavi.

Mrindiko amesema Katika ushirika ambao unanunua mazao Mkoani hapa katavi  kampuni ya GBS haijawahi kuwa na changamoto ya ulipaji hivyo ni chachu Kwa wakulima kuendelea kuzalisha Kwa wingi ili Ili kujikimu binafsi na kukuza uchumi wa mkoa.

This image has an empty alt attribute; its file name is dsc-0319-1024x683.jpg

Mkuu wa mkoa wa katavi Mhe. Mwanamvua Hoza Mrindiko alipokuwa akihutubia wanacnhi wa kijiji cha Makongoro Katika hafla ya uzinduzi wa msimu wa masoko ya Pamba, tumbaku na mazao mchanganyiko. Picha na Festo Kinyogoto

Awali akitoa tathmini ya kilimo kwa mkoa wa katavi kaimu katibu tawala wa mkoa wa Katavi NEHEMIA JAMES amesema mkoa umefanikiwa kizalisha kilo milioni 12 Kwa mwaka huu huku sababu ya uazalishaji huo ukiatajwa kuwa ni uwepo wa Kiwanda kimoja kilichopo halmashari ya wilaya ya Tanganyika pamoja na  maji kituama, magonjwa shambulizi na wakulima kutofuata mbinu za ugani.

This image has an empty alt attribute; its file name is dsc-0305-1024x683.jpg

Kaimu katibu tawala wa mkoa wa Katavi NEHEMIA JAMES wakati akitoa tathini ya kilimo. Picha na Festo Kinyogoto

Kwa upande wao baadhi ya wakulima wa zao hilo wamesema uwepo wa soko Hilo unatoa hamasa ya uzalishaji kwao kwakuwa hawatapata ugumu wa kuuza mazo pale unapofikia muda wa mavuno licha ya kuwa Bei ipo chini hivyo wamewaomba wanunuzi kuongeza Bei ili waweze kunufaika zaidi.

Mrindiko ameagiza kuhakikisha malengo ambayo yanapangwa yanafikiwa Kwa wakulima kufuata mbinu za kilimo, na wataalamu kuhakikisha tathimini inafanyika ili kulinganisha na misimu mingine na kwanini imekuwa vigumu kufikia lengo la kuzaliza Tani milioni 50.

This image has an empty alt attribute; its file name is dsc-0352-1024x683.jpg

Baadhi ya wakulima na wananchi waliohudhuria hafla hiyo. Picha na festo kinyogoto

Back To Top