miongoni mwa Takataka ambazo zipo katika maeneo ya makazi ya watu mtaa wa Mpadeco.picha na…
picha na mtandao
KATAVI
Baadhi ya wananchi wa manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wametoa maoni kuhusiana na maboresho ya barabara yanayoendelea kufanywa na TARURA
Wakizungumza na Mpanda radio FM wamesema kuwa maboresho hayo ya Barabara yakamilishwe kwa wakati
Kwa upande wake meneja wa TARURA Injinia Kahoza Joseph amebainisha kuwa matengenezo hayo yanafanyika kupitia fedha za mpango wa matengenezo ya barabara za tozo za mwaka 2023/2024.
Katika hatua nyingine amewataka wananchi kuhakikisha wanatunza miundombinu inayoboreshwa kwa kuacha kutupa takataka kwenye mitaro, makaravati kwani gharama zinazotumika ni kubwa .