skip to Main Content
mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph akizungumza na waandishi wa habari

Mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph amewapongeza wakulima na wajasiriamali walioenda kwenye maonyesho ya Nanenane jijini Mbeya kwa kuiwezesha halmashauri ya Mpanda kushika nafasi ya tatu katika maonyesho.

Ameyasema hayo wakati akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake ambapo amesema maonyesho ya nanenane yametumika kujifunza mbinu mbalimbali za kilimo pamoja na ufugaji ulio bora.

Sauti ya mkuu wa wilaya

Pia jamila amesema kuwa wilaya ya Mpanda imejiweke mikakati na mipanga katika kuhakikisha ujuzi walioupata kupitia maonyesho hayo unawafikia wananchi wote kwa kuandaa eneo litakalotumika kutoa elimu hiyo kabla ya msimu wa kilimo.

Sauti ya mkuu wa wilaya

Ikumbukwe kuwa maonyesho ya nanena mwaka huu kitaifa yamefanyika jijini Dodoma na kauli mbiu ya mwaka huu ilikuwa Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025.

Back To Top