skip to Main Content

Stesheni ya Mpanda mkoani Katavi .picha na Rachel ezekia

Katavi

Baadhi ya abiria wanaosafiri na treni mkoani katavi wameomba serikali kuboresha huduma zinazotolewa na usafiri huo ikiwemo kuongeza mabehewa  ya abria ,huduma ya kielektroniki ya ukataji wa tiketi.

Wameyasema hayo wakati wakizungumza na mpanda redio fm kwa nyakati tofauti wameeleza namna wanavyopata chngamoto ya vitambulisho katika kupata tiketi kutokana na kutokuwa na vitambulisho vya taifa hasa wakitumia barua kutoka kwa wenyeviti wa mitaa.

Kwa upande wake Emmnueli Mtawali  stesheni master mwandamizi stesheni ya Mpanda ameeeleza katika shughuli zote za usafirishaji kuwa treni mkoani katavi inasafiri mara tatu kwa wiki ikiwa ni pamoja na ukataji wa tiketi katika siku hizo ambazo  abiria wanasafiri amesema kuwa mikakati ya serikali ni kuhakikisha wanaongeza mabehewa ya abiria  pamoja na ukarabati wa njia ya treni.

Stesheni master mwandamizi stesheni ya Mpanda Mtawali  picha na Rachel Ezekia

Katika hatua nyingine ametoa wito kwa abiria kuzingatia taratibu kanuni na sheria za usafiri wa treni kama vile kuwa na vitambulisho ,kufuatilia ratiba za usafiri ,pia changamoto zozote zikitokea ziwasilishwe kwa  stesheni master ili zitatuliwe  kwa wakati.

Back To Top