miongoni mwa Takataka ambazo zipo katika maeneo ya makazi ya watu mtaa wa Mpadeco.picha na…
Tanganyika
Serikali wilayani Tanganyika mkoani katavi imesema kuwa itaendelea kuchukua hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa baadhi ya wananchi wanao vamia maeneo ya hifadhi na mapitio ya wanyama.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya hiyo Onesmo Buswelu wakati akizungumza na mpanda radio fm na kusema kuwa lengo la kutengwa kwa maeneo hayo ni kuendelea kuzilinda rasilimali zilizomo katika eneo hilo
Aidha Buswelu amesema kuwa wilaya hiyo ina maeneo mengi muhimu yanayohitaji ulinzi wa kila mwananchi ili kutokupoteza lengo la serikali la kuendelea kutangaza utalii katika wilaya hiyo.
Wilaya ya Tanganyika ni miongoni mwa wilaya zilizomo mkoani katavi zenye maeneo mengi yanayolengwa na serikali kuendelea kuweka matumizi bora ya ardhi kwa nia ya kulinda rasilimali zilizomo katika wilaya hiyo.