skip to Main Content

KATAVI

Wananchi Halmashauri ya manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wamelaani wazazi wanaoruhusu watoto wadogo kufanya biashara muda ambao walitakiwa wawe shule.

Wakizungumza na kituo hiki wananchi hao wamesema kuwa vitendo hivyo vinaathiri saikolojia za watoto na kuwapotezea malengo yao ya baadae.

Aidha watoto wameainisha sababu zinazowapelekea kujikita kwenye shughuli za utafutaji kuwa ni kukosa mahitaji yao kutoka kwa wazazi hivyo inawalazimu kufanya kazi ili kukidhi baadhi ya mahitaji yao.

Judithi ni Ispector kutoka dawati la jinsia mkoani Katavi, amewataka wananchi kuripoti wazazi wasio watimizia watoto wao mahitaji ya msingi ili serikali iwashurutishe na kuwawajibisha katika suala la malezi.

Back To Top